Sio kitu cha ajabu kusikia wasanii wakiwarusha wanamichezo kwenye ngoma 
zao. Hiki kitu kimeanza muda mrefu sana ndani ya Africa hadi nje ya 
Africa. Mmoja kati ya wanamichezao waliohi kutajwa sana 
kwenye nyimbo za
 HipHop huko marekani ni Michael Jordan au M.J kama wanavyomuita.
Tumeongea na Diamond Platinumz ambapo yeye na wasanii wake wa WCB 
wamekua wakitaja majina ya wana michezo mara kadhaa kwenye ngoma zao 
hasa Ronaldo na Mbwana Samatta.
Diamond tulipomuuliza kuna faida gani kwake na kipi kinamvutia kutaja 
majina ya wachezaji hao kwenye ngoma zake. Jibu lilikua hili “Hata kama 
mtu anafanya kazi kiasi gani kama jamii haijamkubali basi bado ana kazi 
ya ziada ya kufanya hadi akubalike.”
Aliendelea “Sasa mimi nawataja watu ambao wamefanikiwa kukubalika na 
jamii, ukiangalia watu kama Ronaldo na Samatta inaongeza chachu ya 
nyimbo na kupendwa zaidi. Hata wao pia wanafarijika kuona kwamba sisi 
kwa sisi pia tunakubaliana kwa kila kitu tunachofanya.
Jumatano, 4 Januari 2017
New
HILI ni jibu la Diamond kuhusu kwanini anataja majina ya wacheza soka kwenye ngoma zake
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
TUAMBIE