by
HILARY MEDIA
on
15:32
Jumatatu, 31 Machi 2014
New
Jumatatu, 24 Machi 2014
New
TANAZANIAN TWIST
by
HILARY MEDIA
on
15:01
Tanzanian twist
New hit toka DAR SOUND STUDIOS imefanywa na producer Riller, 07130044445
Jumapili, 23 Machi 2014
New
ONGEZA NGUVU ZA KIUME
by
HILARY MEDIA
on
21:06
VYAKULA VINAVYOONGEZA UWEZO KATIKA TENDO LA NDOA
URAFIKI,MAHUSIANO,UCHUMBA NA NDO
Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume na kuacha idadi ya wanawake wanaokabiliwa na tatizo hilo kwa mujibu wa uchunguzi kubaki na asilimia 13.Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili.
Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina kumi ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa. Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:
PILIPILI
Pilipili zilizocheshwa zimetajwa kuwa na uwezo wa kusaidia msukumo wa usambazaji damu mwilini, ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo unaoweza kumfanya mtu akawa na hisia kali za kimapenzi. Kwa msingi huo, ni vema kwa wale wanaokabiliwa tatizo la uwezo wa kufanya mapenzi wakatumia pilipili si kwa wingi bali kwa kiwango stahili, ili waamshe hisia zao.
PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni. Inatajwa kuwa watu wanaotumia tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuonge
za majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.
NDIZI
Wakati unafikiria uwezo wa kufanya vema tendo la ndoa unatakiwa kuwaza juu ya uimara wa misuli ya mwili ambayo inatajwa kuwa ni sehemu kuu na yenye muhimu katika kujamiiana. Kwa msingi huo ulaji wa ndizi mbivu unatajwa kusaidia kujenga misuli mwilini na kumfanya mtu aweze kuwa hodari katika tendo la ndoa.
CHOKOLETI
Ulaji wa Chokoleti huongeza uchangamfu mwilini na, hivyo kumuwezesha mtu anayeshiriki tendo la ndoa kuwa na mguso sahihi kwenye fikra zake, jambo litakalomuwezesha kupokea hisia za mapenzi kwa urahisi zaidi ya mtu ambaye anakwenda kwenye uwanja wa sita kwa sita akiwa mchovu wa mawazo.
CHAZA NA PWEZA
Aina hizi za samaki zinazovuliwa baharini huwa na madini ya zink na chumvi ambayo yanatajwa kusaidia uzalisha wa vichocheo vinavyohamasisha msisimko wa mwili wakati wa tendo la ndoa.
POMEGRANATE
Ni aina fulani ya matunda mekundu yanayofananana na apple. Haya yatajwa kusaidia kuamsha mishipa ya fahamu na kuweka mawasiliano sahihi ya mwili na hivyo kumuongezea mtu uwezo kwa kufanya tendo la ndoa kwa hamasa kubwa.
MVINYO MWEKUNDU
Mvivyo mwenyekundu unatajwa kuwa na uwezo wa kuuchangamsha mwili na kuongeza msukumo wa damu, kiasi cha kumuondolea mtu uchovu kabla na baada ya tendo la ndoa, hivyo ni muhimu kunywewa hasa na wale ambao wanasumbuliwa na tatizo la kushindwa kurudia tendo.
MBEGU ZA MATUNDA
Mchangayiko wa mbegu mbalimbali za matunda, mfano tikiti, maboga husaidia kuondoa ACID mwilini na kumfanya mtu ajione ni mwenye afya njema.
VANILLA
Vanila husaidia kuamasha hamasa mwili.Mwisho wa aina hizi za vyakula ni TIKITI MAJI ambalo linatajwa kuwa na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuusaidia mwili kuwa na nguvu za kutosha kufanya tendo la ndoa
Alhamisi, 6 Machi 2014
New
UTABIRI WA MVUA KUBWA UKANDA WA PWANI
by
HILARY MEDIA
on
12:12
BY MWANANCHI MEDIA
Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania
(TMA), imetabiri kuwa mvua kubwa zitanyesha hasa maeneo ya ukanda wa
pwani huku ikitahadharisha uwezekano mkubwa kusababisha maafa.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi alisema
jana kuwa utabiri huo unaonyesha kuwa maeneo mengi zaidi ya nchi
yanatarajiwa kupata mvua za juu ya wastani... “Hata shughuli za kilimo
zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa kilimo.”
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari TMA pia
imewahadharisha watumiaji wa bahari juu ya mabadiliko ya tabianchi
yanayoweza kusababisha bahari kuchafuka.
Taarifa hiyo imesema kunatarajiwa kuwapo kwa
vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50, kati ya jana na kesho
ambazo zitanyesha mfululizo na kwamba huenda zikasababisha madhara
katika ukanda wote wa pwani.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa mvua hizo
zinasababishwa na kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa Mashariki mwa
Bahari ya Hindi, sanjari na kusogea haraka kwa mvua za masika hivyo
kuongeza kiwango cha unyevunyevu kuelekea ukanda wa pwani.
Mikoa iliyopo katika ukanda huo ambayo inaweza
kuathiriwa na mabadiliko hayo ya hali ya hewa ni Mtwara, Lindi, Pwani,
Dar es Salaam, Tanga na Zanzibar.
“TMA inazitaka mamlaka zinazohusiana na majanga
kuchukua hadhari zinazostahiki ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea
kutokana na mvua hizo,” ilisema taarifa hiyo.
Katika taarifa ya tathmini ya mvua za msimu
kuanzia Machi hadi Mei, mwaka huu iliyotolewa mwishoni mwa wiki
iliyopita, Mamlaka hiyo ilizitaka menejimenti za maafa na wadau wa sekta
ya afya, kuchukua hatua za hadhari kukabiliana na mabadiliko ya
tabianchi yanayoweza kutokea kwa kuwa baadhi ya maeneo yanatarajiwa
kupata mvua za juu ya wastani.
#
meli ya Iran iliyobeba silaha.
Msemaji huyo amesema maroketi hayo yangeiimarisha Hamas kwa kuipa uwezo wa kupiga maeneo karibu yote ndani ya Israel. Meli hiyo ilikuwa ikipeperusha bendera ya Panama, kituo chake cha mwisho kikiwa Port Said nchini Sudan.
Meli za kivita za Israel zinaisindikiza meli hiyo yenye silaha ambayo imebadilishiwa njia na kuelekezwa kwenye bandari ya Eilat nchini Israel. Taarifa za jeshi la Israel zinaeleza kuwa mashirika ya kijasusi ya nchi hiyo yamekuwa yakiifuatilia meli hiyo kwa miezi kadhaa.
New
Israel yaikamata meli ya Iran iliyobeba silaha nzito
by
HILARY MEDIA
on
02:20
Israel yaikamata meli ya Iran iliyobeba silaha.
Israel imesema jeshi lake la baharini limeikamata meli ya Iran katika bahari ya Sham, ambayo ilikuwa ikisafirisha maroketi ya kisasa kwa kundi kipalestina la Hamas linaloudhibiti Ukanda wa Gaza. Msemaji wa jeshi la Israel amesema maroketi hayo ni aina ya M-302 yaliyotengenezwa nchini Syria, ambayo yanaweza kupiga shabaha iliyo umbali wa km 160.
Msemaji huyo amesema maroketi hayo yangeiimarisha Hamas kwa kuipa uwezo wa kupiga maeneo karibu yote ndani ya Israel. Meli hiyo ilikuwa ikipeperusha bendera ya Panama, kituo chake cha mwisho kikiwa Port Said nchini Sudan.
Meli za kivita za Israel zinaisindikiza meli hiyo yenye silaha ambayo imebadilishiwa njia na kuelekezwa kwenye bandari ya Eilat nchini Israel. Taarifa za jeshi la Israel zinaeleza kuwa mashirika ya kijasusi ya nchi hiyo yamekuwa yakiifuatilia meli hiyo kwa miezi kadhaa.