
Staa
 wa Bongo Fleva,Naseeb Abdul’Diamond Platinumz’amewachana wasanii 
wenzake wanaotafuta bifu na yeye na kusema kuwa amesikitishwa na baadhi 
ya wasanii wanaolazimisha kutengezeza ugomvi kilazima bila sababu za 
msingi.

Kupitia
 account yake ya Instagram Diamond aliandika kuwa…kiukweli, nasikitishwa
 sana jinsi baadhi ya wasanii kutwa wanavyolazimisha kunitengenezea 
ugomvi wa kilazima pasipo kuwa na sababu…
Aidha aliongeza kuwa kuna wasanii wengine wamekuwa wakisema kuwa amewatusi kwenye Media, Mara amepost kuwakashifu..
Alimalizia kwa kusema kuwa yaani ilimradi tu....kwanini Wanamuziki wa
 Tanzania Tunashindwa kubadilika... mbona mi nahangaika na muziki wangu 
kimpango wangu... Mnasema nyie ndio mnaojua kuimba mie sijui 
"sinatatizo"... Mnasema nyie ndio wenye sauti nzuri yangu mbaya "Sina 
tatizo"... sasa mbona tena bado mnanifatilia na kutokujua kwangu... 
Nafkiri ni vyema mkaanza kutumia ujuzi wenu kukuza sanaa ya nchi yetu na
 kuleta heshima na maendeleo nchini, kuliko kupika majungu..... Watu 
wanataka kazi!Alimalizia kuandika kwenye Instagram
            
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
TUAMBIE